Wednesday, October 24, 2012

Unapopewa, jiulize unatoa nini? Usiendekeze mapenzi ya kizamani

                          
YACHUKUE mapenzi halafu itazame timu ya mpira wa miguu, kikapu na hata pete (netiboli) inavyocheza. Utaona kwamba ni lazima kupeana pasi mpaka mpira unapomfikia mfungaji. Hakuna mwenye uwezo wa kutoka na mpira golini kwake, akawapita wapinzani 10 na kufunga.
                           
Mpira ni pasi, yaani kushirikiana kutafuta ushindi. Haitakiwi kutegeana. Jinsi unavyoona mpira unavyochezwa, ndivyo na uhusiano wa kimapenzi unavyojengwa. Wewe na mwenzi wako ni timu moja, sasa mnachezaje kutafuta ushindi?
Je, anapokuwa na mpira, nawe unajipanga vizuri ili akupe pasi halafu umrudishie afunge au kazi yako ni wewe kumtazama anavyokatiza na kumshangilia? Anapokabwa na maadui, unakwenda kumsaidia au yako yanabaki macho tu, yaani akidhibitiwa ubaki unasonya, akishinda mshangilie pamoja?

MWANAMME ASHITAKIWA KWA KUMTOBOA, KUMFUNGA KUFULI MKEWE UKENI

 
Mwanamke Sitabai Chouhan akiwa hospitalini.
SIKU ambayo mwanamke Sitabai Chouhan alipolazwa katika Hospitali ya Maharaja Yashwant Raoin huko Indore, India, kwa jaribio la kutaka kujiua kwa kunywa sumu ya panya, ndiyo siku manesi walipogundua kwamba mwanamke huyo alikuwa amefungwa kufuli dogo kwenye mlango wa sehemu zake za siri.
 
Mume wa Sitabai, Sohanial Chouhan.
Mume wake aitwaye Sohanial Chouhan (38) alifikishwa polisi baada ya kugundua kwamba alikuwa ana tabia ya kumfunga kufuli mkewe sehemu hizo kwa muda wa miaka minne kwa madai kwamba asingefanya hivyo angekuwa anatembea nje ya ndoa.

Monday, October 22, 2012

Umetendwa? Futa machozi, tazama mbele, usijilaumu wala usijute

 
Busara, hekima na moyo imara ni vipengele vikuu vitakavyokuwezesha kuvuka changamoto mbalimbali kwenye mapenzi. Fikiria kwamba hata barabara iliyochongwa vema na wahandisi waliobobea, bado milima na mabonde vitakuwepo.
Kama ndivyo, basi inashindikana vipi kutokea kwa hali isiyoeleweka kwenye mapenzi? Ni mambo ya kawaida mno, kwa hiyo busara na hekima viwe ndani yako. Vilevile moyo imara ukupe nguvu ya kuvuka changamoto za hapa na pale.