Tuesday, November 12, 2013

Dk Mvungi Afariki Dunia

Mkurugenzi wa Katiba, Sheria na Haki za Binadamu wa NCCR-Mageuzi, Dk Sengodo Mvungi amefariki dunia leo alasiri nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu baada ya kujeruhiwa na watu wanaosadikiwa ni majambazi.

Taarifa za kifo chake zimethibitishwa na Mwenyekiti Taifa wa NCCR-Mageuzi, James Mbatia.

Dk Mvungi ambaye pia alikuwa Mjumbe wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba alijeruhiwa kwa kukatwa na mapanga kichwani Novemba 13, mwaka huu nyumbani kwake Kibamba Msakuzi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam na kulazwa Taasisi ya Mifupa ya Muhimbili (Moi) na baadaye kuhamishiwa Hospitali ya Milpark, Johannesbarg, Afrika Kusini.

Penzi la Kajala Masanja na Petit Man laota mabawa


 

Habari zilizogazaa mtaani zinasema kuwa  penzi la mwanadada Kajala Masanja na Petit Man Wakuache ambaye ni anafanya kazi na Wema Sepetu kwenye kampuni ya Endless Fame Production limeota mabawa na kwa sasa Petit Man anatoka na mdogo wake Vanessa Mdee.

Kwa mujibu wa The Gossip corp wa clouds FM wawil hao hawapo pamoja tena na mwanadada kajala amejaribu sana kumsihi Petit man wakuache warudiane bila mafanikio

Ray C ajipongeza baada ya kuachana na Mihadarati

MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Rehema Chalamila ‘Ray C’ mwishoni mwa wiki aliandaa sherehe kujipongeza kutimiza mwaka mmoja tangu aanze kutumia dawa za ‘methadone’ ambazo zimemsaidia kupona uraibu uliotokana na matumizi ya mihadarati.

Ray C,aliyabainisha hayo Dar es Salaam juzi, alipokuwa akizungumza na Katibu Mkuu wa Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (Tamisemi), Jumanne Sigini, alipotembelea Kituo cha Tiba cha Dawa za Kulevya (Methadone Wing), kilichopo katika hospitali ya Mwananyamala, Kinondoni.

“Sasa najisikia vizuri na namshukuru baba (Rais Kikwete), kwa kunishauri pamoja na jitihada zake za kuwaleta Wamarekani katika kutupatia tiba hii ambayo imenirudisha katika hali yangu ya kawaida, hadi nikaweza kuingia tena studio kurekodi nyimbo tena, ni jambo kubwa sana na la kujivunia,” alisema Ray C.

HUU NDIO MJENGO ANAOPOROMOSHA MSANII DIAMOND KWA SASA

Kijana anayefanya vizuri kwenye muziki wa Bongo Fleva Diamond Platnumz mambo si mabaya kwake baada ya kuonyesha mjengo wake mwingine wa hatari ambao bado upo katika ujenzi


Kupitia mtandao wa kijamii wa Instagram,Diamond jana ame-share picha ya nyumba hiyo na chini akatia neno..Shuka nayo.

''Toa kitu weka kitu...! Ndio tulivyo funzwa...stareh tunawaachia wajanja wa mji... #WCB #Wasafi for the Fkn Life!''

Haijajulikana mjengo huu uko maeneo gani wala umegharimu kiasi gani ila inaendelea kudhihirisha mafanikio anayoendelea kuyapata Diamond.
 
 
source dj seki 

TAMKO rasmi la Ndugu Zitto Z. KABWE (MB) kuhusiana na kinachoitwa "Taarifa ya Siri ya Chadema"

NILIPOKUWA katika ziara ya bara la Ulaya kati ya Oktoba 21 mpaka Novemba 2 mwaka huu (2013), nilipokea kwa njia ya barua pepe ripoti inayoitwa "Taarifa ya Siri ya Chadema" ambayo pia ilikuwa imesambazwa katika mitandao mbalimbali ya kijamii.

“Taarifa ya Chadema inasema kwamba chama hicho (chama changu) kilikuwa kimechunguza mwenendo wangu tangu mwaka 2008 hadi 2010 na kubaini kuwa mimi napokea fedha kutoka Chama Cha Mapinduzi (CCM) ili kuivuruga Chadema.


Ripoti hiyo ilinihusisha pia na mwananchi raia wa Ujerumani, Andrea Cordes ambaye, kwa mujibu wa ripoti hiyo, alinisaidia kupokea na kuhifadhi kiasi cha dola 250,000 za Marekani kupitia kwenye akaunti yake binafsi.

Tuesday, July 30, 2013

MWANAUME AKATWA ULIMI NA MKEWE KISA WIVU WA KIMAPENZI

Bw.Anord Nyabenda akionesha Ulimi wake namna ulivyokatwa kwa meno na mkewe. Imeelezwa kuwa chanzo ni wivu wa kimapenzi kati yake na mkewe. Hadi sasa mwanamke hajafika Hospitalini alikolazwa kwa matibabu ili kujulia hali mwenzake.

HIVI NDIVYO KABURI LILIVYO FUKULIWA NA MAITI KUIBIWA

 
 
KATIKA hali isiyokuwa ya kawaida, familia ya Said Abdallah inayoishi Buguruni jijini Dar es Salaam imelazimika kutokwa machozi upya baada ya maiti ya mtoto Sophia Said
(1) aliyefariki dunia kwa ugonjwa wa malaria, kuibwa na watu wasiojulikana na kaburi lake kuachwa wazi, Uwazi limechimbua.
Kaburi alipozikwa mtoto Sophia Said likiwa wazi.
Tukio hilo la aina yake na lililoacha maswali mengi, lilitokea usiku wa Julai 20, 2013 kwenye Makaburi ya Buguruni Kwamkanda, Mtaa wa Mnyamani jijini Dar es Salaam. Marehemu alizikwa Juni 20, 2013. Uwazi lilifika eneo la tukio na kukuta umati, ikiwemo familia ya Said ukitokwa machozi huku wakiliangalia kaburi hilo likiwa wazi. Mbao na miti iliyotumika kwenye mazishi ya mtoto huyo vilikutwa pembeni ya kaburi.

Monday, July 8, 2013

JANUARY MAKAMBA AWATAKA WANANCHI WAWALAUMU WABUNGE WAO KUHUSU KODI YA 1000 KWA KILA LAINI.....ADAI WIZARA YAKE ILIPINGA VIKALI


Haya  ni  majibu ya  Naibu Waziri wa Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia Mh. January Makamba akijibu maswali katika mtandao wa Twitter kuhusu kodi mpya ya TZS 1000 kwa mwezi kwa kila line ya simu. 


  •  Amesema kwamba Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia iliipinga kodi hiyo.


  •  Amesema kwamba Hazina (Wizara ya Fedha) walikubaliana na maoni ya Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia kuhusu kodi hiyo.
  • Amesema kwamba Bunge ndilo lililopitisha kodi hiyo na si Wizara ya Mawasiliano, Sayansi na Teknolojia.

Friday, June 28, 2013

NDEGE 8 ZA BARACK OBAMA ZATUA DAR ES SALAAM.


DAR ES SALAAM.   MAKACHERO wa Marekani wameendelea na matayarisho ya mwisho ya ziara ya Rais Barack Obama, ambapo katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere walikuwa na kazi ya kuunganisha helikopta za doria.
Makachero hao walikuwa wakiunganisha helikopta sita zilizosafirishwa vipande vipande kutoka Marekani, ambapo meli mbili za kivita na ndege moja pia zimewasili.
Rais Obama tayari yuko katika ardhi ya Afrika, ambapo leo anatarajiwa kwenda Afrika Kusini baada ya kumaliza ziara yake ya kwanza Senegal na anatar ajiwa kuwasili nchini Jumatatu.
Kwa mujibu wa uchunguzi uliofanywa jana na Mwananchi unaonyesha Marekani imeleta helikopta hizo kwa ajili ya ulinzi wa Rais Obama, zikiwemo meli zilizobeba helikopta nyingine mbili na ndege.
Habari zilizopatikana kutoka kwa wafanyakazi wa Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere,zinasema kuwa helikopta sita zinaunganishwa katika sehemu ya karakana ya Kikosi cha Anga cha Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ).
Mpashaji mmoja aliliambia gazeti hili kuwa helikopta hizo zililetwa kama vipande vipande vilivyosafirishwa kama mzigo kwenye meli za kivita zilizotia nanga jijini Dar es Salaam.
“Nilikaribia kwenye eneo la karakana na nikashangaa kuona jinsi jamaa walivyokuwa ‘bize’ wakiunganisha vyuma mbalimbali na kutengeneza helikopta hizo,” aliongeza mpashaji wetu, ambaye alibahatika kusogelea eneo hilo licha ya kuwepo kwa ulinzi mkali.

Thursday, June 27, 2013

UJIO WA OBAMA OMBA OMBA WAHAMISHWA JIJINI DAR...

 
KAMA UONAVYO KATIKA PICHA HIVI NDIVYO OMBAOMBA WAKIHAMISHWA MAENEO MBALIMBALI YA JIJINI
DAR KUPISHA UJIO WA RAIS OBAMA

HUU NDIO MKWANJA DIAOMND PLATINUM ALIOUINGIZA MWEZI JUNE NA JULY


Staa wa Kesho, Diamond ameendelea kupiga hela kwa show nyingi zinazomfuata kila kukicha. Wingi wa show hizi unazidi kumfanya kuwa miongoni mwa wasanii wachache wa Tanzania wenye pesa nyingi zaidi.
Tumejaribu kuangalia baadhi ya show alizofanya mwezi huu, atakazofanya mwishoni mwa mwezi huu na mwezi ujao ili kukadiria ni kiasi gani anaweza kuwa ameingiza. Baadhi ya show tunafahamu ni kiasi gani aliingiza huku zingine tukikadiria kutokana na jinsi anavyochaji.
Show ya nchini Comoro 22 June

Friday, June 21, 2013

MABOMU ARUSHA; LEMA NUSURA ATUMBUKIE KWENYE MAFUTA YA KITIMOTO

 
Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.

KUFUATIA mapambano ya raia na Jeshi la Polisi mjini hapa, Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (Chadema), Jumanne wiki hii alilazimika kukimbilia kwa wachoma nyama ya nguruwe karibu na eneo hilo ambapo alidaiwa kunusurika kutumbukia kwenye mafuta ya kiti moto.
Lema aliyenusurika kupigwa na bomu lililoharibu gari lake, alikuwa akijaribu kuwatuliza wananchi walioanza kukusanyika katika vikundi, wakijadili amri ya serikali ya kukataza miili ya watu waliofariki dunia katika shambulio la bomu, isiagwe kwenye Viwanja vya Soweto, mjini hapa.
Kabla ya kupigwa mabomu na kukimbilia kwa wachoma nyama ya nguruwe hao, Lema alikuwa akiwataka wananchi kuwa wavumilivu kwani walikuwa wanawasiliana na serikali ya mkoa ili kupata kibali cha kuaga miili ya wapendwa wao.
Ghafla polisi walifika na kutangaza amri ya watu kutawanyika katika viwanja hivyo ili kuweka hali ya usalama ambapo walisema pasingekuwa na suala la kuaga miili ya watu hao katika eneo hilo. Zoezi hilo lilikwama baada ya mabomu kurindima kwa mara nyingine.


source: Global publishers

Wednesday, January 16, 2013

MAMILIONI YA WAUMINI WA DINI YA HINDU WAJISAFISHA DHAMBI ZAO


Hindu
Mamilioni ya waumini wa dini ya hindu wakiingia kwenye mto wanaouita mtakatifu wa Ganges wenye maji ya baridi, kwa kile wanachoamini kunawasafisha madhambi yao
Whip my hair: The holy men presented an arresting sight at the first day of the festival
tayari watu zaidi ya milioni tatu washaingia katika mto huo kwa jana asubuhi na huku wakitegemea kufika watu million 11 kuingia kwenye mto huo kufikia jana jioni,  kwa ushahidi wa afisa mkuu wa maadhimisho hayo, Mani Prasad Mishra
Procession: A child adorned with marigolds is carried by sadhus on the way to the Sangam

PICHA:VIDEO MPYA YA NAY WA MITENGO KUFANYIKA MAKABURINI "WAMENICHOKOZA"

 Msanii rapper wa Bongo Fleva maarufu kama Nay wa mitengo baada ya kutoa ngoma yake inayofahamika kwa jina la Wamenichokoza sasa siku za hivi karibuni ndiyo alikuwa akifanya video ya ngoma hiyo na video hiyo amefanyia maeneo ya makaburini.Kwa hiyo wale mashabiki wa Nay kaa tayari kwa ujio mpya kutoka kwa Nay.

Thursday, January 10, 2013

Ni utata mtupu juu ya kifo cha Jackline Musa Matiko aliyekutwa kafia hotelini

                           
UTATA mkubwa umegubika kifo cha mwanafunzi Jackline Musa Matiko (15) aliyekuwa akisoma katika Shule ya Sekondari Juhudi iliyopo Gongo la Mboto Wilaya ya Ilala aliyekutwa amekufa katika Hoteli ya Southern Resort, Kigamboni Dar es Salaam baada ya wazazi wake kudai kuwa hakufa maji bali alinyongwa.

Akizungumza na gazeti hili mwishoni mwa wiki iliyopita, baba wa marehemu, Mussa Matiku alisema baada ya kuikuta maiti ya mtoto wake kando ya bwawa katika hoteli hiyo na kuichunguza shingo yake aliiona imelegea na tumbo lake halikujaa maji kama watu wanaokufa kwa maji wanavyokuwa.
Alisema kwa vigezo hivyo ni wazi kwamba mwanaye hakufa maji na amelitaka jeshi la polisi kufanya uchunguzi wa kina ili kuwabaini waliomuua kikatili binti yake.
 Naye mjomba wa marehemu ambaye alikuwa na Jackline kabla ya kifo chake aliyejitambulisha kwa jina moja la Abdul, alisema  binti huyo alitoka nyumbani kwa wazazi wake maeneo ya Mazizini Ukonga kwenda Gongo la Mboto kwa bibi yake kusherehekea Sikukuu ya  Mwaka  Mpya.

“Baada ya kufika pale na kupata chakula cha mchana pamoja  na ndugu zake, Ilipangwa kwenda  kutembea kokote walikohitaji ambapo walichagua  kwenda Quality Centre.

WACHINA WAZUIA UPANUZI WA BANDARI YA DAR

 
Waziri wa Uchukuzi, Dk. Harrison Mwakyembe.  

* Waziri Dk. Mwakyembe, Jaji Werema wageuziwa kibao,washitakiwa
WIKI hii kona ya Fumuafumua ilizama bandarini Dar es Salaam na kugundua kuwa shughuli za upanuzi wa bandari kama serikali ilivyokusudia imekwama na kuwa ni ndoto kwa wakati huu.
 
Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Frederick Werema.
Hata hivyo, katika dodosadodosa yetu tumegundua kuwa kuna kesi ambayo imefunguliwa na imezuia muendelezo wowote wa upanuzi wa bandari hiyo ili iwe ya kisasa zaidi.
Imegundulika pia kuwa Kampuni moja ya Kichina iitwayo China Communications and Constraction (CCC) ndiyo iliyoenda Mahakama Kuu, kitengo cha biashara na kuzuia Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kutangaza zabuni ya upanuzi wa bandari hiyo.

Boda boda yaleta timbwili kwa wapendanao MORO

Chanzo chetu hivi karibuni kikiwa kwenye duka la kuuza pikipiki lililopo Mtaa wa Mindu barabara ya kueleka Faya Manispaa ya Morogoro, lilishuhudia pikipiki nyingi zikiwa zimeandikwa ujumbe tofauti.
Kijana mmoja aliyejitambulisha kwa jina la Sule Manga akiwa juu ya pikipiki yake iliyoandikwa maneno yanayosomeka: “Usijisifu una mimba, msifu aliyekutia mimba hiyo” alipoulizwa sababu ya kuandika hivyo alifunguka:

Tuesday, January 8, 2013

KANISA LA AJABU LINALOPINGA BIBLIA TAKATIFU LATUA TANZANIA

Kanisa hilo ambalo linajulikana kwa jina la The Pool of Siloam lililoko Mbezi- Makonde, Kinondoni, Dar es Salaam linafanya ibada zake Jumanne badala ya Jumapili wakiamini ndivyo Neno la Mungu linavyotaka.

Jambo lingine ambalo linachagiza u-ajabu wa kanisa hio…

KANISA lingine la ajabu limegunduliwa Bongo ambapo linafanya ibada zake kwa utofauti mkubwa na makanisa yaliyozoeleka na wengi, Uwazi limechimbua.
                        

PICHA ZA WEMA SEPETU ZIMEMAKE HEADLINE MITANDAO YA JAMII

 
Ikiwa ni mda mchache tu baada ya kupost picha zake zenye kuonyesha wazi sehem za tumbo na kifua kupitia Instagram, picha ya wema imeonekana kusambaa kwa haraka zaidi kupitia mtandao wa jamii "facebook" huku kila mmoja akitoa maoni yake kutoka na mtazamo wake.