Saturday, July 21, 2012

Madada POA watangaza ofa kabla ya mwezi mtukufu kuanza

KATIKA hali ya kushangaza, usiku wa Jumanne iliyopita, chanzo chetu kiliwanasa akina dada wanaojiuza ‘machangudoa’ ambao walisema hawatakuwepo katika eneo la biashara kwa muda wa mwezi mmoja kwa sababu ya Mfungo wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhan.

 Machangu hao walinaswa Corner Bar, Africana Sana- Sinza, jijini Dar es Salaam ambapo walikuwa wakisaka wanaume huku wakidai wanavunja jungu.
Akizungumza na mapaprazi wetu, Rose aliyedai ni kahaba mzoefu wa eneo hilo alisema mara mfungo utakapoanza hata wao watasitisha biashara hiyo mpaka watu wenye imani hiyo watakapomaliza ibada yao.

Unajua nini? Ni kweli tunatenda dhambi, lakini sasa si vizuri wenzetu wafunge halafu sisi tunashughulika na zinaa kwa kuuza mwili, hata Mungu hapendi. Kwa hiyo mimi nitaacha ili kuungana na wenzetu,” alisema Rose, mwenyeji wa Mbeya.

Usiku huohuo, machangu waliokutwa eneo la Kinondoni, jijini Dar nao walisema kwa kipindi hiki cha kuukaribisha mwenzi wa Ramadhan watashusha bei hya huduma hiyo.

1 comment: