Wednesday, September 26, 2012

Ulaya yasitisha msaada kwa Rwanda

                 

                                                        Waasi wa M23  

Muungano wa Ulaya umeamua kusitisha msaada kwa Rwanda.

Uamuzi wa Muungano huo umefikiwa kufuatia ripoti ya baraza la usalama la Umoja huo iliyodai kwamba Rwanda inaunga mkono waasi wa M23 dhidi ya serikali ya Congo.
Waasi hao wanadhibiti kimabavu sehemu kubwa ya Mashariki mwa Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo na hata kuwatoza kodi wananchi.
Kundi hilo lilianza uasi katika eneo hilo mwezi Aprili na kusababisha takriban watu nusu milioni kukimbilia usalama wao.
Lakini Rwanda imeendelea kukana madai hayo.
Umoja wa Mataifa unafanya mkutano na baadhi ya yatakayopewa kipaombele kwenye mkutano huo ni swala la mgogoro huo Mashariki mwa Congo.
Mapema mwezi Julai Marekani ilizuia dola 200,000 zilizokusudiwa kulisaidia jeshi la Rwanda.

Tuesday, September 25, 2012

Mama Rwakatare na Dk. Cheni Presha juu

Nyumba ya Dk. Cheni.
Nyumba ya Mama Rwakatare.

SAKATA la kutangazwa kubomolewa kwa majumba yao kwa sababu tofauti, Mchungaji wa Kanisa la Assembles of God Mikocheni B ‘Milima ya Moto’ la jijini Dar es Salaam, Dk. Getrude Pangalile Rwakatare na staa wa filamu za Kibongo, Mahsein Awadh ‘Dk. Cheni’, sasa presha zao juu.
Kwa upande wa Mama Rwakatare, mjengo wake wa bei chafu aliouzindua hivi karibuni uliopo Mbezi Beach, Dar utavunjwa kwa madai kwamba umejengwa kinyume cha sheria za mazingira kwani upo katika maeneo ya kando mwa mito ya Mbezi Beach, Mndumbwe na eneo maalum la hifadhi ya miti adimu ya Mikoko.

Maaskofu kuwanyima waumini sakramenti


                   
Kanisa katoliki nchini Ujerumani
Sheria kali itakayowashurutisha waumini wa kikatoliki kulipa kodi ya kanisa la sivyo wanyimwe sakramento imepitishwa nchini Ujerumani.
Maaskofu waliopitisha sheria hiyo wamesema kuwa yeyote atakayekosa kulipia kodi ya kanisa ambayo ni asilimia nane ya mapato yao watanyimwa sakramento na kisha kutotambuliwa kama wakatoliki.
Maaskofu hao wameshtushwa na idadi ya watu wanaoendelea kuasi ukatoliki.
Wanasema kuwa hatua kama hii ya kuasi dini itakuwa ni kwenda kinyume kabisa na maadili ya jamii.