Thursday, July 5, 2012

Irene Uwoya akiri kuacha gambe baada ya kuona anapoteza muelekeo

 Irene Pancras Uwoya katika picha

      MWIGIZAJI Irene Pancras Uwoya amekula kiapo mbele ya Ijumaa Wikienda kuwa hataki kuonja pombe tena kwani anakiri zimempotezea mwelekeo kwa kumharibia vitu vyake vingi.
Akizungumza na mwandishi wetu jijini Dar juzikati, Uwoya ambaye ni mke wa ndoa wa mwanasoka wa Rwanda, Hamad Ndikumana ‘Kataut’, alisema amegundua kuwa pombe haina faida kwake.
Tujiunge na Uwoya: “Mbali na kupoteza fedha nyingi lakini wakati mwingine nashindwa kutimiza ratiba yangu na hasa nikiwa na ‘apointimenti’ muhimu nashindwa kuitimiza kwa sababu ya pombe kwa hiyo natangaza rasmi kuacha na nawasihi wasanii wenzangu nao waache.”

No comments:

Post a Comment