Friday, September 21, 2012

Baby Madaha abwaga chakula cha mtoto kwenye kuku wengi

Baby Madaha akiwa jukwaani kuwapa raha mashabiki.
Na Musa Mateja aliyekuwa Morogoro
STAA ‘seksi’ wa filamu na muziki wa Bongo Fleva, Baby Joseph Madaha amejikuta akiumbuka mbele ya mashabiki wake baada ya matiti a.k.a nido zake kuchomoza na kuonekana hadharani akiwa jukwaani na kusababisha midume yenye ukame kumzengea.



...Burudani baada ya kukolea.
Tukio hilo la aibu isiyo na kipimo lilishuhudiwa na mwanahabari wetu usiku wa kuamkia Septemba 17, mwaka huu kwenye Uwanja wa Jamhuri mjini Morogoro ambako kulikuwa na tamasha kubwa la Serengeti Fiesta 2012.
Baby Madaha alifanya kioja hicho baada ya kutakiwa kupanda jukwaani kuimba na Juma Kassim ‘Nature’ ambaye wameshirikiana katika moja ya nyimbo zake.
 
..Baby Madaha akiimba na Juma Nature.
Bila hiyana, Baby alipanda stejini kwa mbwembwe na kujikuta akimwaga ‘lazi’ kwa kuonesha matiti au chakula ya mtoto hadharani na kusababisha umati uliokuwa umefurika uwanjani hapo kulipuka kwa shangwe huku mwanadada huyo akiendeleza libeneke la shoo kali.
 
...Akizidi kujiachia jukwaani.
Baada ya kushuka jukwaani ndipo bidada huyo alipovamiwa na wanaume wakware ambao wakambonyeza ‘Kizenji’ hadi alipookolewa na mabaunsa na kupelekwa nyuma ya jukwaa.
 
...Hapa akaamua kulala kabisa, pembeni ni mkono wa shabiki aliyekuwa akijaribu japo kumgusa mnyange huyo.

No comments:

Post a Comment