Monday, September 17, 2012

MUONEKANO MPYA NA BURUDANI ILE ILE SERENGETI FIESTA MOROGORO BHASSSSSSSS


Nyota wa kizazi kipya katika muziki wa bongo fleva huyu si mwingine ni Ben Pol akionyesha vitu vyake katika stage ya Serengeti Fiesta mkoani morogoro usiku wa kuamkia leo katika viwanja vya jamhuri.
Msanii mwenye miondoko ya pwani huyu si mwingine anajulikana kwa jina la AT akionyesha mambo yake katika jukwaa la Serengeti Fiesta mkoani Morogoro katika viwanja vya jamhuri.
Nyota wa kizazi kipya anayefahamika kwa jina Recho kutoka THT naye alikuwa ni moja kati ya wasanii ambao wametoa burudani ya uhakika kabisa katika tamasha la serengeti fiesta mkoani Morogoro usiku wa kuamkia leo katika viwanja vya jamhuri.
Mwana FA naye ndani ya morogoro Serengeti Fiesta muonekano mpya na burudani ile ile ilizidi kuwashwa na wasanii mbalimbali katika jukwaa la fiesta mkoani Morogoro katika viwanja vya jamhuri
Msanii wa Bongo movie anayejulikana kwa jina la Wema sepetu akionyesha uwezo wake katika jukwaa la serengeti fiesta mkoani Morogoro katika viwanja vya jamhuri.
 Palikuwa hapatoshi Morogoro Serengeti Fiesta katika Viwanja vya Jamhuri maana muonekano mpya na burudani ziliendelea kuwasha moto katika jukwaa la fiesta mkoani hapo.
 Msanii wa kizazi kipya anayetokea katika jumba la vipaji THT huyub si mwingine anafahamika kwa jina la Alini Nipishe akiimba na shabiki wake katika jukwaa la Serengeti Fiesta mkoani Morogoro usiku wa kuamkia leo katika viwanja vya jamhuri.
 Huu umati wa muonekano mpya na burudani ile ile ndani ya morogoro katika viwanja vya jamhuri
 Ommy Dimpozz naye alikuwa ni moja kati ya wasanii ambao wameonyesha vitu vyao katika jukwaa la serengeti fiesta mkoani Morogoro usiku wa kuamkia leo katika viwanja vya jamhuri burudani ile ile bila tatizo na mtu.
Ukipenda Umwite Mwarabu wa Dubai au Bepari la kihaya huyu si mwingine namzungumia Mpoki kutoka Original comedy naye alikuwa ni moja  mpaka  msanii anayejulikana kwa jina la JB akawa anampongeza comedian huyo katika  Tamasha la Serengeti Fiesta mkoani morogoro usiku wa kuamkia leo katika viwanja vya jamhuri.
                                                                   Rich Mavoco
 Msanii wa kizazi kipya akionyesha vitu vyake katika jukwaa la serengeti fiesta mkoani morogoro katika viwanja vya jamhuri usiku wa kuamkia leo.
Dyana akitoa burundani ile ile kwa mashabiki wake katika Tamasha la Serengeti Fiesta viwanja vya jamhuri mkoani Morogoro usiku wa kuamkia leo.
                                                              Ray Vicent Kigosi
Msanii wa Bongo movie akionyesha mambo yake katika jukwaa la serengeti fiesta mkoani Morogoro katika viwanja vya jamhuri usiku wa kuamkia leo.
                      Supa nyota akitoa burudani kwa wakazi wa Morogoro Serengeti Fiesta
                               Muonekano mpya na Burudani ile ile Mwanzo mwisho Morogoro

No comments:

Post a Comment